Quantcast
Channel: g sengo
Viewing all 12422 articles
Browse latest View live

A


S

C

MWANZA IMEJIPANGA HIVI KUFIKIA MALENGO SEKTA YA ELIMU

$
0
0


Ni katika Tamasha la utoaji TUZO ZA UMAHIRI KATIKA ELIMU MKOA WA MWANZA zilizoanzishwa na wadau wa elimu mkoa huo kama sehemu ya mkakati wa kuimarisha na kuongeza kiwango cha ufaulu kimkoa ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Serikali za Mitaa TAMISEMI, Selemani Jafo.

Hizi ni kauli za wasemaji mbalimbali waliopata nafasi ya kuwasilisha mapendekezo yao mbele ya Waziri wa OR TAMISEMI pamoja na halaiki ya hafla hiyo ya tuzo iliyotanguliwa na michezo mbalimbali ya ufunguzi kama chachu ya kujenga mahusiano.

AGIZO LA JPM SHULE YA ISENI B KASI YA UTEKELEZAJI WAKE YAMSHANGAZA JAFO.

$
0
0

AGIZO la Rais John Magufuli alialolitoa Desemba 7, mwaka jana (2019) na kuutaka uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, kujenga madarasa matano katika Shule ya Msingi Iseni B katika Halmashauri hiyo, limetekelezwa kwa zaidi ya asilimia 90.

Akizungumza mwishoni mwa wiki akiwa shuleni hapo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo ameupongeza uongozi wa mkoa na jiji la Mwanza kwa utekelezaji wa agizo hilo uliofanyika ndani ya mwezi mmoja na sasa umefikia hatua ya upauaji.

A

B

KIVUKO KIPYA CHA MV ILEMELA CHASHUSHWA ZIWA VICTORIA KWA MARA YA KWANZA.

$
0
0
TANGU dunia kuumbwa na nchi yetu kupata Uhuru Wananchi wa Kisiwa cha Bezi na Kayenze Mwaloni mkoani Mwanza hawajawahi kuwa na kivuko au usafiri wa uhakika wa meli zaidi ya kutumia mitumbwi na boti ndogo kusafiri na kusafirisha mizigo yao kusaka huduma mbalimbali muhimu.

Hatimaye Leo tarehe 6 mwezi Januari 2020 Ahadi ya Mbunge wa Jimbo la Ilemela Dkt. Angeline Mabula ya kutatua kero ya usafiri wa uhakika kwa wananchi wa visiwa hivyo aliyoitoa kipindi cha uchaguzi mkuu 2015 imetimia baada ya serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, kujenga kivuko chenye uwezo wa kubeba abiria 200, tani 10 za mizigo na magari 10 na kukiingiza majini ziwani Victoria tayari kuanza kutoa huduma ya usafiri. 

 Akizungumza na wananchi hao wakati wa kukiingiza kivuko hicho katika ziwa Victoria, Naibu Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditie amesema kivuko hicho kimejengwa baada ya wananchi kuwasilisha vilio vyao.

Mradi huo umetekelezwa na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano chini ya usimamizi wa Wakala wa Ufundi na Umeme TAMESA baada ya kampuni ya ujenzi na utengenezaji meli ya Songora Marine kushinda zabuni ya utengenezaji wa kivuko hicho.

Mbunge wa Jimbo la Ilemela Angeline Mabula ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi amesema kituo hicho kitafuta machozi ya wananchi huku Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella akiipongeza Serikali kwa ukamilishaji wa ujenzi wa kivuko hicho.

Kukamilika kwa kivuko hicho kunakwenda sambamba  na ujenzi wa vivuko vingine viwili vya Mv Chato na Mv Ukara vinavyotarajiwa kukamilika Februari Mwaka huu ili kuanza kuhudumia wananchi.











 Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampuni iliyotengeneza kivuko hicho ya Songoro Marine Ltd ya jijini Mwanza, Meja Songoro ameishukuru Serikali kwa kuiamini kampuni yake na kuikabidhi tenda kadhaa ikiwemo ya ujenzi wa meli hiyo na nyinginezo nchini kwani kwa mfumo huo, serikali inazidi kuvijengea uwezo viwanda vyake vya ndani.

Awali, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle, akisoma taarifa kwa mgeni rasmi katika tukio hilo alisema serikali kupitia TEMESA inaendelea na ujenzi wa vivuko vingine vipya kwa ajili ya Mafia Nyamisati kwa gharama ya shilingi bilioni 5.3, Bugorola Ukara kwa gharama ya shilingi bilioni 4.2 pamoja na Chato Nkome kwa gharama ya shilingi bilioni 3.1.

Ujenzi wa kivuko cha Mv Ilemela umegharimu kiasi cha bilioni 2.7. 

MAOFISA FEKI WA IKULU WANASWA NA POLISI WAKIWA NA AMBULANCE

$
0
0
🔴Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limefanikiwa kuwakamata watu saba kwa tuhuma za kujifanya maofisa usalama wa Taifa kutoka Ikulu, ambao wamekuwa wakiwatapeli wananchi na baadhi ya watumishi wa serikali katika Jiji la Mwanza.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza ACP Muliro Muliro, amesema matukio hayo yametokea kati ya Desemba 27, mwaka jana na Januari 2, mwaka huu, Nyakato wilayani Nyamagana, walipokuwa wanatumia gari lenye NA. T.751 BNL, aina ya Toyota Ambulance, ambalo walidai ni sehemu ya msafara wa viongozi wakuu.

Kamanda aliwataja Watuhumiwa waliokamatwa ni Chalanga Chalanga (45) Mkazi wa Pasiansi na Arusha Hamis Mwalimu (25) Fundi magari, kujifanya bodygurd wà Chalanga Chalanga, Philipo Petro (35), Mkazi wa Usagara Misungwi, pia dereva wa Chalanga Chalanga, Elia Gunda (30) anayedai yeye ni mchungaji wa Kanisa la EAGT liliopo Kisesa pia Mkazi wa Kisesa. Hassan Juma (29) Mkazi wa Mkolani Fundi wa IT, Seleman Karanga (25), anajifanya Mlinzi Mkuu wa Chalanga Chalanga na Afisa Mkuu wa Ikulu Michael Mazige Mkazi wa Morogoro.

MKWASA ATANGAZWA KUWA KOCHA BORA MWEZI DISEMBA

$
0
0

Kaimu Kocha wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa, ametangazwa kuwa kocha bora kwa mwezi uliopita.


Mkwasa ametwaa tuzo ya ukocha bora ikiwa ni muda mchache tangu achukue nafasi hiyo Yanga baada ya kuondoka kwa Mwinyi Zahera ambaye alikuwa anaiona timu hiyo.

SADIO MANE ASHINDA TUZO YA MCHEZAJI BORA WA AFRIKA 2019 🏆 JUU YA SALAH NA MEHREZ

$
0
0


Mshambuliaji wa Liverpool Sadio Mane amenyakuwa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka 2019, katika sherehe iliyofanyika usiku uliopita nchini Misri katika eneo la ufukwe wa Hurghada.
.
Mane amemshinda mchezaji mwenzake wanayekiputa klabu moja Mohamed Salah wa Misri na Mahrez aliyeiongoza Algeria akiwa nahodha katika michuano ya kombe la mataifa ya Afrika yakiyofanyika mwaka jana nchini Misri na anayekiputa katika klabu ya #ManchesterCity 

✂HII HAPA ORODHA YA WACHEZAJI WANAOUNDA KIKOSI CHA FifPro Africa Best XI  FOR 2019

Andre Onana (GK) 🇨🇲
Serge Aurier 🇨🇮
Joel Matip 🇨🇲
Kalidou Koulibaly 🇸🇳
Achraf Hakimi 🇲🇦
Idrissa Gana Gueye 🇸🇳
Riyad Mahrez 🇩🇿
Hakim Ziyech 🇲🇦
Mohamed Salah 🇪🇬
Pierre-Emerick Aubameyang 🇬🇦 
Sadio Mané 🇸🇳

#CAFAwards2019

MSANII WA KENYA ATUNGA WIMBO KUMHUSU RAIS WA TANZANIA.

KIONGOZI MUADHAMU : TUMEMPIGA KIBAO TU ADUI, ANACHOPASWA MAREKANI NI KUONDOKA ENEO HILI.

$
0
0
Kiongozi Muadhamu: Tumempiga kibao tu adui, anachopaswa kufanya Marekani ni kuondoka eneo hili
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, mashambulio ya makombora yaliyofanywa na Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH katika kambi mbili za Marekani nchini Iraq ni kibao cha uso tu alichopigwa adui huyo.
Amesema, majibu ya Iran hayatoishia hapo kwani kinachotakiwa hasa ni kuangamizwa kikamilifu uwepo wa kifisadi na kiharibifu wa Marekani katika eneo hili zima.
Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema hayo leo asubuhi (Jumatano) wakati alipoonana na maelfu ya wananchi wa Qum na huku akitilia mkazo uhakika kwamba mataifa ya eneo hili na tawala zilizotokana na wananchi, bila ya shaka yoyote hazitaki kuona Marekani inaendelea kuwepo katika eneo lao, amesema, kuwepo Wamarekani kwenye eneo hili na katika sehemu yoyote ile duniani hakuna matokeo mengine isipokuwa vita, ugomvi, fitna na kuharibiwa miundombinu ya eneo hilo.

Vile vile amezungumzia nafasi ya kipekee isiyo na mbadala ya Luteni Jenerali Qassem Soleimani katika kufelisha njama za Marekani huko Palestina, Iraq na Lebanon na kuongeza kuwa, shahid Luteni Jenerali Soleimani alifanikiwa kuvunja na kufelisha njama zote za Marekani zilizotumia fedha nyingi, mabavu, uchochezi wa kisiasa na uundaji wa makundi mbalimbali.
Ayatullah Khamenei ameongeza kuwa, tunaposema "adui" tunakusudia Marekani, utawala wa Kizayuni na majimui ya vibaraka wao na kuongeza kuwa, baadhi ya tawala za ndani na nje ya eneo hili hazipaswi kuingizwa kwenye kundi hilo la adui hadi pale zitakapochukua hatua ya kumtumikia adui.
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu pia amesisitiza kuwa, muswada uliopasishwa na bunge la Iraq wa kufukuzwa wanajeshi wa Marekani nchini humo ni hatua nzuri sana na tunamuomba Mwenyezi Mungu alete taufiki ya kuendelea jambo hilo katika nchi nyinginezo.

WHO: UGONJWA WA SURUA ULIUA WATU 6000 NCHINI DRC, 2019.

$
0
0
WHO: Ugonjwa wa surua uliua watu 6000 nchini DRC, 2019

Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwa, watu 6,000 walipoteza maisha kufuatia mlipuko wa ugonjwa wa surua (measles) nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, mwaka uliomalizika 2019.

WHO imetoa mwito wa kupatiwa fedha zaidi ili kupambana na mlipuko huo unaoaminika kuwa mkubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Kufikia sasa, WHO imeweza kupokea dola milioni 27.6 za Marekani, ingawaje inahitaji dola milioni 40 zaidi ili kupanua shughuli ya kutoa chanjo kwa watoto kati ya miaka 6 na 14, katika kipindi cha miezi sita ijayo.

Dakta Amedee Prosper Djiguimde, afisa wa Shirika la Afya Duniani nchini Kongo DR amesema, "Maelfu ya familia za Wakongomani wanahitaji misaada yetu ili kuzikwamua kutoka kwenye mgogoro huo wa kiafya. Hatuwezi kufanya chochote iwapo hatuna fedha."

Chanjo ya surua
Kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF), asilimia 74 ya wagonjwa hao wa surua ni watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano na mbaya zaidi ni kuwa, takribani asilimia 90 ya vifo ni watoto wa umri huo.
Takwimu zinaonyesha kuwa katika mwaka uliomalizika wa 2019, takribani maambukizi laki 3 yanayodhaniwa kuwa ni ya surua yaliripotiwa.

KITUO CHA PILI NCHINI CHA KUPIMA NA KUHAKIKI MATENKI YA MALORI YA MAFUTA CHAANZA KUFANYA KAZI MWANZA

$
0
0


WAMILIKI wa Malori ya kubeba mafuta kwa mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Mara, Kagera, Simiyu, Geita na mikoa jirani na Kanda ya Ziwa sasa hawato ingia gharama ya kuchoma mafuta kusafirisha maroli yao hadi jijini dar es salaam kwaajili ya kupata huduma ya upimaji na uhakiki matenki yao kila mwaka mara baada ya Serikali kusimika kituo cha kisasa cha upimaji katika eneo .la Nyamhongolo wilayani Nyamagana jijini Mwanza.Hiki ni kituo cha pili cha upimaji matenki ya magari ya kubebea mafuta nchini kikitanguliwa na kile cha jijini Dar es salaam.Meneja wa wakala wa vipimo mkoani Mwanza Arobogast Kajungu anasema malengo ya Serikali katika kuwahudumia wafanyabiashara wa mafuta Kanda ya Ziwa yametimia.

MFUMUKO WA BEI MWEI DISEMBA 2019 WABAKI KUWA ASILIMIA 3.8

$
0
0

Kaimu Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii Bi. Ruth Minja akizungumza wakati akitangaza mfumuko wa bei wa mwezi Desemba 2019.
Na Mwandishi Wetu
Mfumuko wa Bei wa Taifa kwa mwaka ulioishia mwezi Desemba, 2019 umebaki kuwa asilimia 3.8 kama ilivyokuwa  mwezi Novemba, 2019.
Akizungumza na waandishi wa habari  leo Jijini Dodoma wakati akiwasilisha taarifa ya hali ya mfumuko wa bei, Kaimu mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii Bi Ruth Minja amesema kuwa mfumuko wa Bei wa mwezi Desemba, 2019 umebaki kuwa sawa kama ilivyokuwa mwezi Novemba,2019 hali iliyochangiwa na kuongezeka na kupungua kwa bei za baadhi ya bidhaa za vyakula na bidhaa zisizo za vyakula kwa kipindi kilichoishia  Desemba, 2019 ikilinganishwa na mwezi Desemba 2018.
“Baadhi ya bidhaa za vyakula zilizoongezeka bei kwa mwezi Desemba, 2019 zikilinganishwa na bei za mwezi Desemba 2018 ni pamoja na;mchele asilimia 7.0, mtama kwa asilimia 3.3, nyama kwa asilimia 2.3, maharage asilimia 7.7, na viazi mviringo kwa asilimia 2.7”; alisisitiza Minja
Akifafanua amesema kuwa bidhaa zisiszo za vyakula  kwa mwezi  Desemba 2019zilipungua bei ikilinganishwa na mwezi Desemba, 2018, Bidhaa hizo ni pamoja na gesi ya kupikia kwa asilimia 2.1, mafuta ya taa kwa asilimia 7.1,jiko la kupikia la gesi kwa asilimia 1.6, mafuta ya petrol I asilimia 8.7 na dizeli asilimia 8.7.
Mfumuko wa Bei wa bidhaa za Vyakula na Vinywaji Baridi kwa mwaka unaoishia mwezi Desemba, 2019 umeongezeka kwa asilimia 6.3 kutoka asilimia 6.1 kwa mwaka unaoishia mwezi Novemba, 2019.
Aidha, Mfumuko wa Bei wa Taifa kutoka mwezi Januari 2019, umepungua hadi  asilimia 3.4 mwaka 2019 kutoka asilimia 3.5 mwaka 2018.
Kwa upande mwingine, Wastani wa Mfumuko wa Bei wa Bidhaa zisizo za vyakula kwa mwaka 2019 ulipungua hadi asilimia 4.0 kutoka asilimia4.3 ilivyokuwa mwaka 2018.
Kwa upande wa nchi ya Kenya mfumuko wa Bei kwa mwezi Desemba, 2019 umeongezeka hadi asilimia 5.82 kutoka asilimia 5.56 kwa mwaka ulioishia mwezi  Novemba,2019, Wakati nchini Uganda kwa mwezi unaoishia Desemba,2019 mfumuko wa bei umeongezeka hadi asilimia 3.6 kutoka asilimia 3.0 kwa mwaka unaoishia mwezi Novemba 2019.

MBUNGE ATEKELEZA AHADI YA USAFIRI WA BAISKELI KWA VIONGOZI UWT UKEREWE

$
0
0



Mbunge atekeleza ahadi ya usafiri wa baiskeli kwa viongozi wa Jumuiya ya Wanawake(UWT) Wilaya ya Ukerewe ngazi ya Kata zote 25 ambazo wataxiyumia kusaka kura za Rais Dkt John Pombe Magufuli, Wabunge na Madiwani na kuhakikisha CCM inashinda kwa kishindo mwezi Oktoba mwaka huu. 

PICHA ZOTE NA PETER KATULANDA.

WAZIRI KIGWANGALLA NA KATIBU WAKE WAMALIZA TOFAUTI ZAO KWA KUMWAGA NEEMA HII YA UTALII MWANZA

BODABODA WAFURAHIA SERIKALI KUWAKUMBUKA KUINGIZWA MFUKO WA BIMA YA AFYA (NHIF)

$
0
0

Jumuiya za Wajasiriamali wadogowadogo na Waendesha Bodaboda nchini wamepongeza hatua ya kuanzishwa kwa vifurushi vya bima ya afya ambavyo vimewawezesha katika kupata matibabu ya uhakika pindi wanapoumwa. Wakiongea wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha wananchi kujiunga na vifurushi vya Bima ya Afya viongozi wa jumuiya hizo wamesema ilikuwa ni hitaji lao la muda mrefu la kuhakikisha wanachama wao wanakuwa na uhakika wa matibabu kwa kuwa na bima za afya. Aidha Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya Mhe. Anne Makinda akiongea wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha wananchi kujiunga na vifurushi vya bima ya afya Mkoani Mwanza, ambapo alisema mpango wa vifurushi umekuja kwa ajili ya kuwajumuisha watanzania wote.

MKURUGENZI MKAZI WA BENKI YA DUNIA AANAYEMALIZA MUDA WAKE BI.BELLA BIRD APONGEZA TASAF KWA MAFANIKIO YA KUPUNGUZA UMASKINI NCHINI.

$
0
0
 Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF ,Bw. Ladislaus Mwamanga  (picha ya juu na chini ) akimkabidhi zawadi Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia anayemaliza muda wake nchini Bi. Bella Bird katika hafla ya kuagana naye .
 
 Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Bw. Ladislaus Mwamanga (aliyesimama) akizungumza wakati wa hafla fupi ya kuagana na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia aliyemaliza muda wake, Bi. Bella Bird alipofika kwenye ofisi ndogo za Mfuko huo jijini Dar es Salaam kuagana na wafanyakazi wa taasisi hiyo.
 Baadhi ya wafanyakazi wa TASAF wakimsikiliza Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Bi. Bella Bird (hayupo pichani ) wakati alipofika katika taasisi hiyo kuagana nao baada ya kumaliza muda wake nchini.


Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF bw.Ladislaus Mwamanga (aliyevaa tai) akimwongoza Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia anayemaliza muda wake bi. Bella Bird kuingia katika ukumbi wa mikutano wa TASAF katika ofisi ndogo jijini Dar es Salaam.


Na Estom Sanga- TASAF- DAR ES SALAAM

Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia anayemaliza muda wake Bi.Bella Bird amepongeza jitihada za serikali ya Tanzania kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii- TASAF- kwa hatua inazoendelea kuchukua katika kukabiliana na umaskini nchini.

Bi.Bella Bird amesema Tanzania imepata mafanikio makubwa katika azma ya kuwaondolea wananchi wake kero ya umaskini jambo ambalo amesema limeijengea heshima kubwa serikali na hivyo kufanya mataifa mengine hususani ya bara la Afrika kuwavutiwa nayo. 

Mkurugenzi Mkazi huyo wa Benki ya Dunia anayemaliza muda wake ameyasema hayo alipokutana na Wafanyakazi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii –TASAF- katika Ofisi ndogo ya Mfuko huo jijini Dar es salaam ambako alikwenda kuagana nao baada ya kumaliza kipindi chake cha takribani CHA utumishi wa miaka minne hapa nchini. 

‘’ mataifa mengine ya Afrika yamekuwa yakija Tanzania kujifunza namna TASAF ilivyofanikiwa kuwafikia watu maskini kabisa kupitia Mpango wake wa Kunusuru Kaya Maskini’’ amesisitiza Bi. Bella Bird. 

Amesema tafiti huru za ndani na nje ya nchini zilizofanywa zinaonyesha kuwa umaskini nchini Tanzania umepungua katika kipindi cha utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini na kuwa kinachotakiwa sasa ni kuhakikisha kuwa mafanikio hayo yanalindwa, kuboreshwa na kuendelezwa. 

Bi.Bella Bird amesisitiza kuwa Benki ya Dunia itaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika utekelezaji wa miradi inayolenga kuboresha maisha ya wananchi na kuongeza kuwa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaotekelezwa na Serikali kupitia TASAF ni miongoni mwa miradi hiyo. 

Akizungumza katika hafla hiyo fupi Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Bw. Ladislaus Mwamanga ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa kuweka mazingira yaliyosaidia Benki ya Dunia kukubali kufadhili shughuli za Mpango was Kunusuru Kaya Maskini. 

Bwana Mwamanga amesema mafanikio makubwa yaliyopatikana katika utekelezaji wa shughuli za Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini ya sehemu ya kwanza yamewezesha Serikali kukubali kutekeleza sehemu ya pili ambayo inatarajiwa kuzinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli baadaye mwezi ujao. 

Mkurugenzi Mtendaji huyo wa TASAF ameahidi kuwa taasisi hiyo imejipanga vizuri kuhakikisha kuwa sehemu ya pili ya Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini inatekelezwa kwa ufanisi mkubwa kwa kuzingatia maelekezo ya Serikali huku Mkazo ukiwekwa katika kuwashirikisha Walengwa katika kutekeleza miradi ya Maendeleo kwenye maeneo yao na kisha kulipwa ujira kama sehemu ya kuwaongezea kipato . 

Utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF ulianzishwa na Serikali kwa lengo la kusaidia wananchi kupitia utaratibu wa Kaya Maskini sana ili ziweze kujikimu kwa kupata mahitaji muhimu yakiwemo lishe, elimu na afya huku mkazo ukiwekwa katika kuziwezesha kaya za Walengwa kutumia sehemu ya ruzuku kuanzisha miradi midogo midogo ya uzalishaji mali ili kuinua kipato chao na kuboresha maisha yao. 
Viewing all 12422 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>